9058010082

9058010082



Tamthilia katika onyesho la kwanza, inajaribu kueleza hali na uhusiano wa kiuchumi baina ya bara la Afrika na la Ulaya. Ame na Zidi wanajadiliana juu ya mihogo iliyovunda, isiyofaa na jinsi ya kuitayarisha iii iweze kulika Baadaye tunawaona wakishindwa kuikata na kuichoma, na hivyo kulazimika kuila tu kinyama.

Maisha ya binadamu kulinganishwa na ya wanyama ni kigezo cha ubwege. Mwanadamu amepotea njia na kujitoma katika ulimwengu wa kinyama Haya ni maisha mabaya, machafu mithili ya kiumbe wa kiubwege Wanyama hawana uwezo wa kuboresha maisha yao sawa na Ame na Zidi ambao tunaambiwa hawana kisu wala kibiriti ambacho kingewasaidia kutayarisha chakula chao (uk 10-11)

Hata hivyo, hali hii ni fumbo kuhusu hali mbaya ya biashara kati ya mataifa ya Ulaya na ya Kiafrika Waafrika, inabainika, wanahitaji vitu vingi zaidi kutoka Ulaya huku nchi za Kimagharibi zikisawiriwa kama zilizoendelea sana na kujitosheleza kimahitaji. Aidha, Waafrika wanasawiriwa kama watu wajinga ambao hawataki kufikiria na kujizatiti kuvumbua vitu vyao Kwao, muhimu ni kulała, kuzembea kazi na kumtegemea Mzungu kwa yote. Zidi anasema:

Kwanza yanaumiza kichwa, pili, utafikiri kipi wewe Mwafrika ambacho Wamarekani, Waingereza, Warusi, Wafaransa na Wajerumani hawajakifikiria? Tatu, si vipo tu vitu vyenyewe duniani vimeenea? Na sisi tunanunua tu Huu ulimwengu wa biashara ati! (uk. 10)

Hii ni hali inayobainika bayana hata hapa nchini mwetu, ni hali ya kiuhalisia Ubwege urno katika maisha ya Waafrika (Ame na Zidi). Wahusika hawa hawana uwezo wala nia ya kutekeleza wajibu wao wa kikazi licha ya kupatiwa mazingira yenye rutuba, na malighafi muhimu.

37



Wyszukiwarka

Podobne podstrony:
Katika onyesho la nane, Ame na Zidi wanakubali kuwa mazingira ya maisha yao ni duni lakini lewa vile
Wimbo wanaoimba Ame na Zidi katika onyesho la tatu unaendeleza majivuno ya Waafrika Rangi nyeusi ina
Tamthilia ya Amezidi inabainisha mazingira ya kibunilizi yenye ishara mbalimbali za kiuasilia Onyesh
TAN BI HI Mlama P. M. (1983)    “Utunzi wa tamthilia katika Mazingira ya Tanzania”.
2.5.5 DRAMA YA KIUBWEQE 0ARąN! AFRIKA Uandishi wa drama ya kiubwege n; mpya katika eneo hili la Afri
WESOŁE DYKTANDA KLASA 3 1 DECYZJA WILKA . Raz na hali na Pod..,.alu wilk prjgm....wfi pełen ....
str31 DECYZJA WILKA Raz na hali na Pod alu wilk przem....wił pełen alu: - Coraz go. ..ej wieść tu ..
tyco2 Tyco Electronics Polska Sp. z o.o. serdecznie zaprasza do odwiedzenia stoiska 55 w hali 5 Na t
Zadania z rachunkowości zarządczej Zad.4. Przedsiębiorstwo Cedr produkuje 3 wyroby w jednej hali, na
Kotwica0167 328 11. Stężenia konstrukcji drewnianych głych i umieszcza się je wzdłuż hali na wysokoś
Anio?y,obywatelki,kokietki i?mony ?niel Kalinowski 128 Poś wia towska, Hali na (1995) Wierne un/bmn
Anio?y,obywatelki,kokietki i?mony ?niel Kalinowski 128 Poś wia towska, Hali na (1995) Wierne un/bmn
P5050428 366 Budynki halowe i obiekty o specjalnym przeznaczeniu dachu, a z drugiej na kratownicy ob
Anio?y,obywatelki,kokietki i?mony ?niel Kalinowski 128 Poś wia towska, Hali na (1995) Wierne un/bmn
Kundi la kwanza lilijikita zaidi katika matumizi ya yaliyomo katika tamthilia kudhihirisha dhana ya

więcej podobnych podstron