9365206695

9365206695



Wimbo wanaoimba Ame na Zidi katika onyesho la tatu unaendeleza majivuno ya Waafrika Rangi nyeusi inaonewa fahari na wahusika hawa ingawa umuhimu wake haudhihiriki bayana. Ni wimbo ambao mtunzi anautumia baada ya kumsawiri Mari Mari ni mhusika ambaye amekengeuka kiasi cha kudharau na kutotambua mambo na hali ya bara la Afrika, bara lakę. Mari anathamini na kutukuza ya Mzungu Wimbo huu basi unaelekea kuwakashifu Waafrika wanaodunisha hali yao kwa kufuata ya kigeni Ame na Zidi wanaimba:

Tunaimba wimbo huu Wimbo wa fahari na makuu Tunaimba kuisifu rangi hii ya fuu (wanaonyesha ngozi zao)

(uk. 27)

Huu ni wimbo wa kiuhalisia, hauna maudhui ya kiudhanaishi Hali ya Waafrika ambao ni maskini, kutegemea na kufurahia visivyo vyao kama magari, vifaru, mavazi na vyakula, ni dhahiri. Hata hivyo, mwishoni mwa wimbo huu, tunapata miale ya ubwege Taswira ya watu wazembe na wasio na uwezo wa kutekeleza lolote lenye manufaa ila kungojea majaaliwa hubainika. Wanatuambia:

Na kazi, ya nini kazi?

Haina haja kazi!

Ya nini uvumbuzi?

Tu huru: tumejitawala!

Tuna kila kitu kwa fedha zetu Tuvumbue, tuvumbue nini?

Tutawalipa wanaovumbua...

Wanaotuvumbulia (uk. 28)

Ni wimbo unaokejeli Waafrika kwa kujidai kuwa wako huru huku wakiendelea kumtegemea Mzungu Aidha, unatupatia picha inayokaribiana na ya Vladimir na Estragon katika Waiting for Godot. Wahusikia hawa wanasawiriwa kama vibonzo kwa kukaa, kupiga domo ovyo ovyo huku wakimngojea Godot Ni wahusika ambao hawana hata uwezo wa kuvua viatu (uk 9).



Wyszukiwarka

Podobne podstrony:
Katika onyesho la nane, Ame na Zidi wanakubali kuwa mazingira ya maisha yao ni duni lakini lewa vile
Tamthilia katika onyesho la kwanza, inajaribu kueleza hali na uhusiano wa kiuchumi baina ya bara la
Badała ya Ame na Zidi kufanya kazi, wanatumia wakati wao mwingi kulała na kuzungumza. Suala hili la
Nlohamed anatumia mbinu ya mhusika ndani ya mhusika katika tamthilia ya Amezidi. Ame na Zidi wanabad
Ame: Nafsi yako. Zidi: Nafsi yangu imefanyaje? Ame: Inajicheka. Zidi: Labda inajicheka au inatucheka
Ptsis (1) — Zb.OS.ŹOjS -*L a (z) ^ame*n.c /na V _x , /I i / jlj Z (s) - ) Ul$)
16741 Ptsis (1) — Zb.OS.ŹOjS -*L a (z) ^ame*n.c /na V _x , /I i / jlj Z (s) - ) Ul$)
— 122 — mamle donner et legue son ame k Dieu son crćateur et i la Bcnoiste Vierge Marie et k tous le
kama kazi ya kiubwege Ubwege ni tapo la kifasihi linalofuata falsafa ya udhanaishi Mwingiliano huu k
kama kazi ya kiubwege Ubwege ni tapo la kifasihi linalofuata falsafa ya udhanaishi Mwingiliano huu k
Tamthilia ya Amezidi inabainisha mazingira ya kibunilizi yenye ishara mbalimbali za kiuasilia Onyesh
Aidha, tunapata ‘Wimbo wa Mzee’, wimbo ambao sawa na dondoo kutoka Kilio cha Haki, unapitisha haja y
Tukimulika wimbo wa Mwalimu na Wanafunzi tunapata maudhui yanayopingana na mkabala wa kiubwege Wimbo
Mbuzi aliyekosa majani ni jazanda ya Waafrika wanaokufa kwa njaa kwa sababu ya ukame na vita vya wen

więcej podobnych podstron