9058010041

9058010041



kama kazi ya kiubwege Ubwege ni tapo la kifasihi linalofuata falsafa ya udhanaishi Mwingiliano huu kati ya ubwege na udhanaishi ndio sababu tosha iliyotusukuma kutumia udhanaishi kama chombo cha kuabiria katika utafiti wetu.

Baadhi ya sifa za ubwege ambazo zinaoanisha mada yetu na nadharia tunayoitumia ni suala la mandhari Mandhari hujitokeza kama nguzo ya kukuzia vipengele vingine vya udhanaishi Ubwege hutilia maanani mazingira ya fasihi. Kiubwege, mazingira yanayobainishwa huwa ni machafu na ambayo huchukiza. Hali hii hulengwa kuashiria kuchukiza kwa maisha. Suala hili linaingiliana vizuri na imani ya kidhanaishi kuwa maisha ni adhabu, hayana furaha. Albert Camus (Cruickshank 1959:27) anadai kwamba furaha ya kudumu haiwezi kupatikana katika maisha ya binadamu, maisha yake ni ya huzuni tupu.

Udhanaishi unatazama hali ya binadamu kama ambayo ni duni na ambayo haiwezi kutamanika. Kwa wana-udhanaishi, furaha ni neno lingine la adhabu.

Umuhimu wa suala la mandhari katika fasihi ya ubwege, unasisistizwa na Mbatiah (1997:8) anaposema kuwa katika fasihi ya uduni (Literaturę of The Absurd), suala la mandhari ni muhimu sana Wasanii katika tapo hili, hutumia mandhari kubainisha msimamo wao kwamba ulimwengu ni wa kinasibu, duni na wa kukatisha tamaa na yanazua hisia za uchovu, huzuni na kukata tamaa

Fasihi ya ubwege huwa haina muumano mzuri wa vitushi ambao ndio mhimili wa ploti. Hivyo basi matukio yake huwa yamevurugwa kiasi cha kutoweza kuyaunganisha. Mambo hutokea tu

kiupweke, ni kama kila jambo limejitenga Utengano huu wa vitushi katika kazi za kiubwege, unaenda sambamba na imani ya kidhanaishi kwamba binadamu ni kiumbe pweke, na aliyejitenga na wenzake pamoja na jamii yake. Anajikuta katika ulimwengu dhalimu bila msaada wowote Greene (1960:1) anaeleza kuwa kinachotambulika ulimwenguni ni hali ya kukata tamaa, hofu na upweke ya kuweko kwa binadamu

Wahusika wa"kazi za kiubwege, huwa hawana uwezo wa kuboresha hali zao Vitendo vya mhusika huwa havina muwala wala umuhimu wowote ila kuonyesha ubatili tu. Mambo madogo madogo kama kutoa viatu, kutembea na kupika, yanawashinda. Hali hii ndiyo

18



Wyszukiwarka

Podobne podstrony:
kama kazi ya kiubwege Ubwege ni tapo la kifasihi linalofuata falsafa ya udhanaishi Mwingiliano huu k
Badała ya Ame na Zidi kufanya kazi, wanatumia wakati wao mwingi kulała na kuzungumza. Suala hili la
n° 233 • aout 2004 • 2 • liullclin ile liaismi ct tVinfornMtion il n y a eu ni mort, ni blessś, la p
80803 Zdjęcie1280 (4) ukoWO* ****, Wwh Jut pb*^*** ni(i
rok Rok sł. D. Komiński, muz. K. Bayer4 i i i JJ 1J J J~31 IJ J j jjlj ka - ni - ze - la. pan Rok S
Elimu katika ulimwengu wa mabwege hukosa misingi thabiti ya kijamii Mara nyingi huwa ni elimu ya kui
Mbuzi aliyekosa majani ni jazanda ya Waafrika wanaokufa kwa njaa kwa sababu ya ukame na vita vya wen
Ni wahusika wanaovalia matambara licha ya kuwa na mazingira yenye mbolea na malighafi chungu ozima.
lastscan22 2 fi p= b. pj E rf TT »ni / k Lotu- la i Y>
13444 strona0013 (3) ni Miii la /.i-hiowukn I l .ofln Mnhska C. Bur t, powtarzając badania Spearmana
Atlantę geopoliticodcllo spazio post-sovictico 0)11 fi ni cconflitti I O I T t I C I LA SCUOLA
ObrazE098 b nami izoymi Slupami egzocyklicznymi. Tymiwa i cylozyaa są pirymidy-—ni {rys. la); każda

więcej podobnych podstron