9058010100

9058010100



Elimu katika ulimwengu wa mabwege hukosa misingi thabiti ya kijamii Mara nyingi huwa ni elimu ya kuigwa na ambayo haisaidii binadamu kuboresha maisha yake, bali husaidia katika kumwangamiza zaidi.

Katika tamthilia ya Amezidi, Mwalimu na Wanafunzi wake wanalala darasani na kati yao,

hakuna anayeweza kumwokoa mwenzake kutoka janga la kutojua. Ni hali ambayo inazidi

kubomoa nchi ya Amezidi kwa kukosa viongozi wenye ujuzi wa kuleta maendeleo. Hali hii

¥

hukaribiana na tunayopata katika tamthilia ya Ionesco, The Lesson Mhusika Pupil, anapatiwa elimu ambayo haimsaidii kukua wala kuimarisha maisha yake, elimu anayopata inamnyooshea mkono wa maangamizo, kifo Mwandishi anatupatia elimu isiyo na maana kwa jamii ndiposa Pupil, anauawa na Professor.

Katika onyesho la nne, tunaonyeshwa dhahiri matatizo yanayoikumba sekta ya elimu barani Afrika. Nchi ya Amezidi, inafuata mfumo wa elimu ya kigeni ambao haufungamani na mazingira yake Tunaambiwa na Mwanafunzi

Hivi ... hivi baada ya kukariri mawazo ya Archimides kwa miaka mingi, kwa nini hatujaweza kuunda nyambizi?

(uk. 30)

Ni swali ambalo viongozi wa Kiafrika wanapaswa kujibu, lakini hata wao hawana mwelekeo, ni mabwege. Mwalimu hajui jibu lakę ndiposa wanafunzi pamoja naye, wanalia na kucheka kuashiria mtafaruku wa mtazamo wa elimu hii Hapa tunapatiwa Mwalimu ambaye tunatarajia amepata mafunzo ya kutosha kuelekeza wanafunzi, lakini anashindwa kutekeleza wajibu wake Anafundisha mada ambayo haielewi na kushindwa kujibu maswali ya wanafunzi Ni mwalimu asiyefuata maadili ya ualimu Anasinzia darasani kuonyesha ubwete wake Aidha, anaingia darasani na bakora ndefu. Labda bakora ni silaha yake ya kuogofya baadhi ya wanafunzi wasimwulize maswali na kumsumbua kichwa. Mazingira ya darasani yanachukiza:

46



Wyszukiwarka

Podobne podstrony:
Aidha, inabainika kuwa hadithi ya watu wanaoishi katika ulimwengu wa kidhahania wa kufikirika tu ina
Wahusika wa kiubwege hukosa historia. Katika tamthilia ya Amezidi, wahusika tunaopewa hawana ukuaji
Politechnika Wa rszawska Wariz IM Ci imamm • u- KI VII WAMAWSKIŁ l>NI TtCMNIj«k ugryźć
3.0 SURA YA TATU 3.1    UTANGULIZI Katika sura hii tumedhamiria kuonyesha jinsi tamth
nuty1 URODZINY marchewki Melodia ludowa Wa mar-(hew-ki u - ro-dn-ny ze-siły wszystkie się ja-rzy-ny.
M1 ■137- WA £ ptźcżtnie i l. se^yia. iV Zoo A £f ]/
Mtindo wa tamthilia zetu umetokana na ule wa fasihi ya Kiingereza ambayo ililetwa kwetu na elimu ya
Badała ya kufikiria kifo kama mwisho wa maisha, napendekeza tukitazame kama kitendo cha mwisho
TAN BI HI Mlama P. M. (1983)    “Utunzi wa tamthilia katika Mazingira ya Tanzania”.
2.5.5 DRAMA YA KIUBWEQE 0ARąN! AFRIKA Uandishi wa drama ya kiubwege n; mpya katika eneo hili la Afri
Tamthilia katika onyesho la kwanza, inajaribu kueleza hali na uhusiano wa kiuchumi baina ya bara la
Kuchanganyikiwa kwa mfumo wa elimu ya Kiafrika unabainika zaidi, tunapopatiwa sauti ya redio Mazingi

więcej podobnych podstron