9365206676

9365206676



Aidha, inabainika kuwa hadithi ya watu wanaoishi katika ulimwengu wa kidhahania wa kufikirika tu inafanana na ngano ya pango la Plato4 Kwa mujibu wa Ayi Kwei Armah, ngano ya pango la Plato inatamba hadithi ya watu waliofungwa na minyororo na kuishi katika kiza cha pango katika kipindi cha maisha yao yote. Ilitokea kuwa, mfungwa mmoja alipata nafasi ya kutoka nje ya pango na akawahi kujionea uzuri na utamu wa jua. Mfungwa huyo aliporudi pangoni, aliwaelezea wenzake juu ya mwangaza na ubora wake lakini hakuna aliyemwamini.Mwenye kuona mwangaza alidharauliwa na kuitwa mzushi na mwehu .

Ngano hii imetolewa kufundisha jamaa kuwa watu wanaoishi katika mazingira na hali tofauti za kilimwengu huwa na maono tofauti. Wale wanaoishi katika ulimwengu finyu kimawazo hawana uwezo wa kufikiria na kuona mambo yaliyoko nje ya duara lao finyu.

Hali hii ndiyo hubainika katika tamthilia ya. Amezidi. Wakazi wa nchi ya Amezidi wamekubali ulimwengu wao duni na kuukabidhi maana za kipekee na ambazo hazieleweki nje ya muktadha wao. Pango, kwao ni kasri zuri lililosheheni ubora wa kisasa. Katika tamthilia hii, pango linapatiwa maana za aina yake Kadhia nyingi zinazohusu maisha ya raia wa Amezidi zinaigizwa pangoni Mazingira haya ni ya kuchukiza na yana nia ya kuashiria uduni.uchafu na maisha yasiyokuwa na thamani- maisha ya Mwafrika.

Mohamed anabadilisha badilisha pango lakę na kulipa mandhari tofauti ya kimawazo Taswira ya pango machoni mwa wasomaji hugeukageuka kutegemea madhumuni ya mwandishi Onyesho la kwanza na la pili kwa mfano huashiria uasili wa Mwafrika. Pango linaashiria hali isiyobadilika ya maisha ya bara la Afrika. Ni bara ambalo halijaendelea kiteknolojia wala kurutubisha historia ya wakazi wake. Tunaambiwa :

Tendo hili lote linatokea ndotoni mwa Ame

na zidi ...pahaia ni palepale pangoni!

Aidha, tunaambiwa kuwa,

(kaketi chini kwenye majani ambayo ni godoro

lakę. Anamtikisha :idi.)Aimka bwana. siku ngapi zirnepita9

(uk 12)

76



Wyszukiwarka

Podobne podstrony:
Elimu katika ulimwengu wa mabwege hukosa misingi thabiti ya kijamii Mara nyingi huwa ni elimu ya kui
Katika onyesho la nane, Ame na Zidi wanakubali kuwa mazingira ya maisha yao ni duni lakini lewa vile
Inabainika kuwa. Mohamed ameathiriwa na mtazamo wa kiubwege Kiubwege, wahusika hawaendelezwi kihisto
2.5.5 DRAMA YA KIUBWEQE 0ARąN! AFRIKA Uandishi wa drama ya kiubwege n; mpya katika eneo hili la Afri
3.0 SURA YA TATU 3.1    UTANGULIZI Katika sura hii tumedhamiria kuonyesha jinsi tamth
Mtindo wa tamthilia zetu umetokana na ule wa fasihi ya Kiingereza ambayo ililetwa kwetu na elimu ya
Wimbo wanaoimba Ame na Zidi katika onyesho la tatu unaendeleza majivuno ya Waafrika Rangi nyeusi ina
Haya ni maisha ya kukatisha tamaa kwa umma Ni maisha ambayo hayatoi matumaini kwa watu wapenda maend
Badała ya kufikiria kifo kama mwisho wa maisha, napendekeza tukitazame kama kitendo cha mwisho
Mohamed anakiuka mwelekeo huu kwa kuwapa wahusika wake wazo ia wokovu kutoka kwa Mungu Katika sura y
TAN BI HI Mlama P. M. (1983)    “Utunzi wa tamthilia katika Mazingira ya Tanzania”.
Fasihi ya ubwege hujaribu kubainisha ukweli juu ya maisha ya binadamu ulimwenguni Webb (1972:23) ana
Kundi la kwanza lilijikita zaidi katika matumizi ya yaliyomo katika tamthilia kudhihirisha dhana ya
Tamthilia katika onyesho la kwanza, inajaribu kueleza hali na uhusiano wa kiuchumi baina ya bara la

więcej podobnych podstron