9058010023

9058010023



Uchambuzi huu umetufaa kwa kutupatia miale ya mawazo ya waandishi wa kibwege licha ya kwamba haukuzama wala kutumia mikakati ya kitaalamu

Sarara (1997)6 ameshughulikia maudhui katika tamthilia tatu za Said Ahmed Mohamed -Pungwa (1988), Kivuli Kinaishi (1990), na Amezidi (1995). Uhakiki huu umetoa mchango kwa utafiti wetu licha ya kwamba mhakiki amejikita katika maudhui tu, na kwamba kipengele cha ubwege hakijitokezi katika kazi yake

Njogu na Chimerah (1999) wametoa maelezo kuhusu Amezidi kama tamthilia ya kibwege. Wamebainisha na kufafanua kwa kifupi baadhi ya vipengee vinavyoendeleza ubwege kama vile wahusika, tamaa na matumaini. Ni kazi ambayo imenufaisha utafiti wetu ingawa wachambuzi hawakutumia nadharia yoyote

Uhakiki wowote ule una manufaa yake. Hivyo basi hatuwezi kupuuza mchango wa wenzetu kama Vuzo, Maneno, na Wafula, ambao wamejikita zaidi katika maudhui na fani. Hivi ni vipengee muhimu chambilecho Ngara (1990:5) ambaye anasema kuwa iii kuelewa kazi ya sanaa, msomaji anapaswa kufahamu yaliyomo na fani yake.

Ni matumaini yetu kuwa, kwa kutumia nadharia mahususi, sisi tutapiga hatua kubwa zaidi mbele katika kuihakiki tamthilia ya Amezidi kama kazi ya kiubwege

1.8 MSINGI WA KINADHAR1A

Nadharia ni chombo muhimu kwa mhakiki kwa vile ndiyo hutoa mwongozo bora wa utafiti Utafiti wetu utaelekezwa na kuongozwa na nadharia ya udhanaishi.

A Dictionary of Literary Terms (1977: 251) inafafanua udhanaishi ifuatavyo:

Kwa misingi ya kifalsafa, udhanaishi hujikita

katika maoni ya hali na maisha ya mwanadamu, mahali pakę na jukumu lakę katika dunia pamoja na mahusiano yake, au ukosefu wa mahusiano hayo na Mungu. (Tafsiri yetu)

11



Wyszukiwarka

Podobne podstrony:
Mohamed anakiuka mwelekeo huu kwa kuwapa wahusika wake wazo ia wokovu kutoka kwa Mungu Katika sura y
Mohamed anakiuka mwelekeo huu kwa kuwapa wahusika wake wazo ia wokovu kutoka kwa Mungu Katika sura y
kuenea kwa mawazo ya kijinga ya Mwafrika hata baada ya kifo cha viongozi wao Mwandishi hapa anadunis
Binadamu anaugua kutokana na maambukizo ya huzuni; amefanywa bubu kutokana na kuporomoka kwa&nb
4.7 PLOTI Ploti kwa kifupi ni ule msuko wa vitushi na namna vitushi hivyo vinavyosababishana; ni seh
Haya ni maisha ya kukatisha tamaa kwa umma Ni maisha ambayo hayatoi matumaini kwa watu wapenda maend
Mawazo haya ya Sartre na Nietzsche juu ya Mungu, yalikuwa yamedhihirika awali hasa kupitia Pascal (F
kama kazi ya kiubwege Ubwege ni tapo la kifasihi linalofuata falsafa ya udhanaishi Mwingiliano huu k
Kuchanganyikiwa kwa mfumo wa elimu ya Kiafrika unabainika zaidi, tunapopatiwa sauti ya redio Mazingi
Mlu habadiliki kiasi hiki kwa siku moja Bila shaka Mari ameonja ya ulimwengu tangu aondoke kijiji ch
Mbuzi aliyekosa majani ni jazanda ya Waafrika wanaokufa kwa njaa kwa sababu ya ukame na vita vya wen
Binadamu anaugua kutokana na maambukizo ya huzuni; amefanywa bubu kutokana na kuporomoka kwa&nb
kama kazi ya kiubwege Ubwege ni tapo la kifasihi linalofuata falsafa ya udhanaishi Mwingiliano huu k

więcej podobnych podstron